Karibuni NL Internet C@fe kwa huduma safi ya internet yenye kasi ya 5mbps kupandisha na kushusha.Tupo Tabata CCM,mkabala na kituo cha mafuta cha OILCOM.

Wednesday, March 21, 2012

MMOJA AFARIKI, 14 WAJERUHIWA KATIKA AJALI YA BASI LA PRINCE MURO HUKO SENJELE-TUNDUMA


Basi la Prince Muro baada ya kupata ajali.…

Maradhi ya Ajabu


MTOTO Honolata Juma Christian (8), (pichani) mkazi wa Mgeta wilayani Mvomero aliyetelekezwa na ndugu zake kutokana na maradhi ya ajabu yanayo msumbua, http://www.blogger.com/img/blank.gifanataabika katika hospitali ya rufaa mjini hapa akiomba msaada wa shilingi 1,000,000 ili akatibiwe.
Gharama hizo ni za tiba,usafiri na matumizi katika Hospitali ya KCMC ya mjini Moshi ambako ameshauriwa kwenda na madaktari wa hospitali ya Mkoa wa Morogoro alikolazwa.
Honolata ambaye tangu kuzaliwa kwake amekuwa akisumbuliwa na magonjwa likiwemo la kuota nywele mwili mzima, nundu mbili kichwani mithili ya pembe na matatizo ya macho.
Mtoto huyo analelewa na mama yake mzazi, Grace Francis (30) ambaye anadai ndugu zake wamemsusia na hawataki kumsaidia.

Monday, February 27, 2012

Saturday, February 18, 2012

JK aongoza matembezi ya hisani kusaidia ujenzi wa hospitali ya kinamama ya CCBRT jijini Dar


Rais Kikwete akiongoza matembezi ya Hisani kuchangia ujenzi wa hospitali ya kinamama ya Baobab iliyo chini ya CCBRT jijini Dar es salaam. Katika picha kutoka kulia Meya wa Ilala Mh Jerry Silaa, Meya wa Kinondoni Mh Mwenda, Bw Erwin Telemans Mkurugenzi mtendaji wa CCBRT, Rene Meza Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya CCBRT Bw. Wilbroad Slaa na kulia kwa Rais ni Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dr. Hadji Mponda na Mkurugenzi wa Vodafone Foundation Bw. Andrew Dunnet pamoja na Mwamvita Makamba wa Vodacom Tanzania katika matembezi hayo leo asubuhi.

JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA LAWAMANI KUHUSIKA NA KIFO CHA MWANACHUO ALIYE FARIKI SIKU YA WAPENDANAO YANI VALENTINE DAY






Marehemu Daniel Godluck Mwakyusa (31) ambaye ni mwanafunzi wa chuo cha TEKU aliyeuawa na Askari wa Jeshi la Polisi PC Maduhu tarehe 14/02/2012 katika sikukuu ya wapendanao {valentine day].

Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.

Watu watatu wamefariki dunia mkoani MBEYA katika matukio matatu tofauti, likiwemo la tukio la Mwanafunzi wa chuo kikuu cha TEKU kilichopo jijini mbeya marehemu Daniel Godluck Mwakyusa (31) ambaye ni mwanafunzi wa chuo hicho aliuawa na Askari wa Jeshi la Polisi PC Maduhu tarehe 14/02/2012 katika sikukuu ya wapendanao {valentine day].

Marehemu akiwa na wenzake wanne walikuwa katika matembezi ambapo polisi walikuwa doria walikuta vijana hao wakipata vinywaji ndipo waliwatuhumu kuwa ni majambazi ambapo PC Maduhu alimpiga marehemu risasi mbili kwa kutumia bunduki aina ya [SMG].

Pia marehemu aliporwa shilingi laki tatu pamoja na simu ya mkononi .

Kwa mujibu wa baba mzazi wa marehemu huyo Bwana Pastory Mwakyusa amesema kuwa anasikitishwa sana na kitendo hicho kilichotokea kwani mwanawe hakuwa na tabia ya wizi au ujambazi hivyo ameliomba Jeshi la Polisi kueleza sababu ya kumuua mtoto wake.

Hata hivyo Jeshi la Polisi lilitoa usafiri wa gari lenye nambari za usajili T 138 AFK aina ya Coster kwa ajili ya kusafirisha Mwili wa marehemu kwenda katika wilaya ya Kyela kwa ajili ya mazishi baada ya uchunguzi wa daktari kuthibitisha kuwa marehemu ameuwawa kwa risasi.

Tukio la pili marehemu Zuberi Mwajeleba (21) mkazi wa kijiji cha Ibumba wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya ambaye alinyongwa kisha mwili wake kutupwa katika mto wa Kanyegele wilayani humo.

Kamanda wa polisi mkoani Mbeya Advocate Nyombi amesema chanzo cha tukio hilo bado hakijafahamika na Jeshi la Polisi linaendelea kufanya uchunguzi juu ya tukio hilo.

Katika tukio la tatu limetokea majira ya saa nane mchana katika eneo la Ilomba jijini Mbeya ambapo pikipiki yenye namba za usajili T 834 BOX aina ya Shinray ambayo dereva wake bado hajafahika alimgonga mtoto Mildred Immanuel (10) mkazi wa eneo hilo.

Hata hivyo dereva alitoroka na kuitelekeza pikipiki katika eneo la tukio na pikipiki hiyo imehifadhiwa katika Kituo cha kati cha Jeshi la Polisi, na mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa Jijini Mbeya na Polisi wanafanya juhudi za kumtafuta dereva huyo.

HABARI YA KUFUFUKA.
Wakati huo huo katika hali isiokuwa ya kawaida Roza Simbeye ambaye ni mama wa mtoto mmoja katika kitongoji cha Isandula, kijiji cha Vuwile, Kata ya Isandula, aliyefariki Februari 16 majira ya saa kumi na mbili za jioni amefufuka wakati taratibu zote za mazishi zipokamilika kama kuchimba kaburi na kuchonga jeneza na taratibu za ibada.

Na ilipofika majira ya saa 3:30 asubuhi ya Februari 17 baada ya kaburi kuchimbwa na jeneza kukamilika zilianza taratibu za kuchukua mwili wa marehemu Roza chumbani ndipo watu waliopewa jukumu la kumwosha walishangaa kumwona marehemu akiwa hai huku akiwa amtoa macho kama vile mtu ametoka usingizini ambapo mpaka sasa kaburi halijafukiwa wala jeneza halijatumiwa na kufanya wanakijiji kubaki na mshangao.

JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA LAWAMANI KUHUSIKA NA KIFO CHA MWANACHUO ALIYE FARIKI SIKU YA WAPENDANAO YANI VALENTINE DAY


Marehemu Daniel Godluck Mwakyusa (31) ambaye ni mwanafunzi wa chuo cha TEKU aliyeuawa na Askari wa Jeshi la Polisi PC Maduhu tarehe 14/02/2012 katika sikukuu ya wapendanao {valentine day].

Happy Nenga ilivyotaka kutumaliza


Mungu ni mkubwa sana na bado anapenda niishi, hii ajali ckutegemea kama kuna mtu angepona, nilikuwa na kaka yangu tunatoka mbeya kuja dar siku hiyo... tumefika mitaa ya inyara (Tazama Pipeline) basi la ngangaline lilisimama njiani likipakia abiria na sisi tulikuwa kwenye mwendo wa kasi sana akashindwa kuova take ikabidi aliweke pembeni kwa kuseleleka na kukaa mkao huo..... but we are alive.

Saturday, February 4, 2012

We're better off than United, and Torres can prove it, says Villas-Boaz


Nice to see you? When you are a Chelsea manager under fire, surely the last person you would want stalking the training ground is owner Roman Abramovich (right), yet that was Andre Villas-Boas¿s fate on Saturday as he prepared to face United

Read more:

Friday, January 27, 2012

BALAA! SERIKALI YASHUPAA MADAI YA MADAKTARI


Na. Aron Msigwa –MAELEZO
Serikali imewataka madaktari wote nchini walio kwenye mgomo kurejea katika vituo vyao vya kazi na kufanya kazi za utabibu ili kuokoa maisha ya wagonjwa.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Hadji Mponda amesema serikali inatambua mchango walio nao wataalam wa afya katika utoaji wa huduma za afya nchini na inaendelea kuboresha maslahi yao.
Amesema serikali kwa kutambua mchango huo imekuwa ikiboresha maslahi yao na kuongeza nafasi za ajira kila mwaka kwa wataalam wenye sifa kutoka nafasi 1,677 za mwaka 2005/2006 hadi kufikia 9,391 katika mwaka huu wa fedha 2011/2012.
“Serikali inatambua mchango wa watumishi wa kada za afya nchini na ndio maana nafasi za ajira zimekuwa zikiongezeka kila mwaka hasa katika mwaka huu wa fedha 2011/2012”
Amefafanu kuwa madaktari kupitia Chama chao (MAT) wamewasilisha madai mbalimbali serikalini yakiwemo nyongeza ya posho ya kuitwa kazini baada ya kazi na madaktari kupewa nyumba za kuishi karibu na hospitali amesema kuwa serikali imekuwa ikifanya jitihada za kuboresha maslahi hayo ili kuwawezesha wataalam hao kutekeleza majukumu yao ikiwemo ujenzi wa nyumba 8 za madaktari kwa wilaya 18 pamoja na kufanya maboresho ya posho.
“Serikali imepata fedha kutoka Mfuko wa Dunia(Global Fund) kwa ajili ya kujenga nyumba za madaktari na kwa kuanzia wilaya 18 zilizo pembezoni zimechaguliwa kujengewa nyumba 8 kila wilaya kama hatua ya kuboresha upatikanaji wa nyumba”
Kuhusu malipo ya udhamini kwa madaktari wanaochukua mafunzo ya uzamili,Kuhamisha madaktari bingwa wenye mikataba ya Ajira na Hospitali ya Taifa Muhimbili, Posho ya mazingira hatarishi na ajira za madaktari amesema kuwa baada ya serikali kupandisha hadhi ya hospitali za mikoa kuwa hospitali za Rufaa za mikoa kumekuwa na umuhimu wa madaktari hao kwenda kufanya kazi katika hospitali hizo na kuongeza kuwa idadi ya udhamini wa madaktari katika mafunzo ya uzamili imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka.
Aidha kuhusu madai ya kutaka nyongeza za mishahara ya shilingi milioni 3.5 kwa mwezi Dkt. Mponda ameeleza kuwa mishahara ya watumishi serikalini hufuata miundo ya utumishi (Scheme of Service)iliyopo huku akibainisha kuwa muundo wa malipo ya watumishi wa umma katika sekta ya afya umeboreshwa.
“Lazima tukubali kuwa baada ya kuboreshwa kwa miundo ya utumishi wa umma wafanyakazi wa sekta ya afya hivi sasa wanapata mishahara mikubwa kuliko watumishi wengine serikalini” amesisitiza.

MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ATEMBELEA MASHAMBA YA MPUNGA KOROGWE, AWEKA JIWE LA MSINGI JENGO LA UKUMBI NA OFISI YA HALMASHAURI YA KOROGWE


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka Jiwe la Msingi katika jengo jipya la Ukumbi na Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe, wakati alipokuwa katika ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo ya Wilaya ya Korogwe mkoa wa Tanga jana Januari 26, 2012.

Majambazi yapanga mawe na kupora manyoni


Ndugu zangu,

Niliondoka Singida Mjini saa kumi na moja alfajiri kuelekea Dodoma. Kilomita 40 kutoka Manyoni nilikutana na hali hiyo pichani kunako saa kumi na mbili na nusu. Eneo la tukio niliwakuta askari watano wamevalia kiraia wakiwa na silaha za moto. Wameniambia tukio limetokea usiku wa kuamkia leo majira ya kuanzia saa sita usiku na linawahusisha maja majambazi wasiopungua wanane.

Kuna walioporwa fedha, simu na mali zao . Mahali hapa kuna pori kubwa upande wa kushoto. Inaaminika majambazi hayo yenye silaha yangali yamejiicha porini.
Hakuna aliyekamatwa. Nilishuhudia polisi hao wakifuatilia nyayo huku wakinionyesha mahali majambazi hayo yalilala chini kujificha wakisubiri giza na kuanza kupanga mawe yao. Kwa kusoma mazingira ya eneo kwangu mimi napata tafsiri kuwa majambazi hayo yalifanya maandzi ya mpango wao kwa siku kadhaa.

Maana, mawe hayo mazito yanaonekana kuwa yalikuwa yakisogezwa usiku karibu na tukio na kufikia idadi waliyohitaji. Intelijensia ya kipolisi ingefanya kazi yake sawa sawa na kwa kushirikiana na wenyeji ingewezeza kubaini mapema movement ya mawe yale. Na katika dunia ya sasa , mbwa wa polisi waliopewa mafunzo wangefanya kwa haraka na kwa ufanisi zoezi la kufuatilia majambazi porini badala ya polisi kufuatilia nyayo kwa macho

mtoto waua Mbeya


Mwili wa marehemu ilvia Isaya (5) alieuawa kisha viungo vya mwili wake kunyofolewa ulimi, jicho la upande wa kushoto, sehemu za siri na mguu wake wa kushoto kuvunjwa ukiwa umefunikwa kwa kitenge, kutokana na kuharibika vibaya hivyo kushindwa kuuonesha.

MWANAMKE ASHITAKIWA KWA KOSA LA KUSABABISHA KIFO CHA MWANAE

Habari na Mwandishi wetu
Neema Edson mwenye umri wa miaka 19 mkazi wa Namtanga Swaya jijini Mbeya amefikishwa katika mahakama ya mkoa kwa kosa la kumuua mtoto wake akiwa mchanga.

Akisoma shitaka hilo mbele ya hakimu mkazi mfawizi Monika Ndyekobola mwanasheria wa serikari Ema Msofe amesema mshtakiwa alitenda kosa hilo January 3 mwaka huu maeneo ya namtanga jijini hapa.

Amemtaja mtoto aliyeuawa kuwa Steven Chinga ambaye alikuwa na umri chini ya miezi kumi na miwili kinyume na kifungu cha sheria namba 199 sura ya 16 kama kilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.

Hata hivyo mshtakiwa hakutakiwa kujibu lolote kutokana na mahakama hiyo kutokuwa na dhamana ya kusikiliza kesi kama hizo na kesi hiyo itaanza kusomwa upya februari 6 mwaka huu katika mahakama kuu.