Saturday, May 19, 2012
Mtoto wa Ajabu -songea
MTOTO mwenye maumbile ya ajabu akiwa na jinsia mbili za kiume na moja ya kike amezaliwa Aprili 25 mwaka huu majira ya saa 11 jioni katika hospitali ya mkoa wa Ruvuma mjini Songea. Mtoto huyo ambaye bado yupo hai chini ya uangalizi maalum amezaliwa akiwa na hitilafu katika maumbile yake ikiwa ni pamoja na kuzaliwa na nusu ya ubongo ambayo imetokana na hitilafu kwenye mfumo wa kichwa hadi uti wa mgongo.
Muuguzi wa zamu katika wodi ya wazazi katika hospitali ya mkoa ambako mtoto huyo anaangaliwa Agness Mwinuka amesema mtoto huyo ambaye amezaliwa na uzito wa kilo moja na gramu 900 amezaliwa akiwa na jinsia mbili za kiume na jinsia moja ya kike.
“Jinsia moja ya kiume ipo kama kawaida isipokuwa jinsia moja ya kiume ipo kichwani karibu na kisogo na jinsia ya kike ipo utosini, mtoto huyu tangu azaliwe juzi hadi sasa hana uwezo wa kunyonya wala kula kitu chochote, uchunguzi wa kitabibu bado unaendelea’’,alisisitiza.
Mama mzazi wa mtoto huyo Situmahi Mwinuka(32) mkazi wa Msamala mjini Songea anasema huyu ni mtoto wake wa nne kuzaliwa na kwamba watoto wake wengine watatu hawajawahi kupata hitilafu yeyote katika mwili.
Kaimu mganga mfawidhi wa hospitali ya mkoa wa Ruvuma Dk.Mathayo Chanangula akielezea hali ya mtoto huyo alisema mtoto anakabiliwa na tatizo ambalo kitaalam ni hitilafu kwenye mfumo unaoanzia kichwani hadi kwenye uti wa mgongo ambao umesababisha mtoto huyo kuzaliwa na nusu ya ubongo.
Kulingana na daktari huyo hitilafu hiyo imesababisha mifumo ya mwili kuwa na dosari ambapo kuna sehemu mbili za kiume moja ikiwa kichwani na kwamba mtoto anapolia sehemu ya kiume ya kichwani inasimama na kusisitiza kuwa maisha ya mtoto huyo ni mafupi kutokana na mifumo ya mwili wake kutokamilika licha ya kwamba mtoto amezaliwa na miezi tisa.
“Katika nchi zilizoendelea madaktari bingwa na wenye vifaa vya kisasa wanaweza kuokoa maisha ya mtoto huyo,hata kama mtoto huyo anaokolewa atakabiliwa na tatizo kubwa la ulemavu wa akiri kwa kuwa ubongo alionao ni nusu tu ya ubongo unaotakiwa kwa binadamu kamili’’,alisisitiza.
Dk. Chanangula anabainisha kuwa mama mjamzito anaweza kujifungua mtoto mwenye maumbile ya ajabu iwapo atakosa madini aina ya folic acid ambayo alisisitiza ni muhimu kwa mama mjamzito kunywa madini hayo miezi mitatu ya mwanzo ya ujauzito wake.
“Mama anaweza kujifungua mtoto mwenye maumbile ya ajabu iwapo katika miezi mitatu ya mwanzo katika ujauzito wake atatumia dawa aina ya flagile, dawa za minyoo, tetesakline na baadhi ya dawa za malaria kama vile SP ambayo anaruhisiwa kunywa baada ya wiki 28 na ALU ambayo hairuhusiwi kabisa kutumika kwa mjamzito kwa ujumla ni marufuku mama mjamzito kunywa dawa bila kumuona daktari’’,alisisitiza.
Katika hospitali ya mkoa wa Ruvuma hili ni tukio la kwanza la aina yake mtoto kuzaliwa akiwa na hitilafu kubwa katika mifumo ya mwili wake.
Habari hii imeandikwa na Albano Midelo
Sunday, May 6, 2012
BARAZA JIPYA LA MAWAZIRI HILI HAPA WAZEE
===== ===== ===
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
ORODHA YA MAWAZIRI NA NAIBU MAWAZIRI
MAWAZIRI
1. OFISI YA RAIS
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mahusiano na Uratibu)
Ndugu Stephen M. Wasira, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, (Utawala Bora)
Ndugu George Mkuchika, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (UTUMISHI)
Ndugu Celina Kombani, Mb.,
2. OFISI YA MAKAMU WA RAIS
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MUUNGANO)
Ndugu Samia H. Suluhu, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (MAZINGIRA)
Dr. Terezya P.L. Huvisa, Mb.,
3. OFISI YA WAZIRI MKUU
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji na Uwezeshaji)
Ndugu Mary M. Nagu, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Hawa Ghasia, Mb.,
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge)
Ndugu William V. Lukuvi, Mb.,
4. WIZARA
Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Ndugu Samuel J. Sitta, Mb.,
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
Ndugu Shamsi Vuai Nahodha, Mb.,
Waziri wa Ujenzi
Dr. John P. Magufuli, Mb.,
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii
Dr. Hussein A.H. Mwinyi, Mb.,
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Dr. Shukuru J. Kawambwa, Mb.,
Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
Ndugu Sophia M. Simba, Mb.,
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Ndugu Bernard K. Membe, Mb.,
Waziri wa Katiba na Sheria
Ndugu Mathias M. Chikawe, Mb.,
Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Ndugu Emmanuel Nchimbi, Mb.,
Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
Dr. David M. David, Mb.,
Waziri wa Kazi na Ajira
Ndugu Gaudentia M. Kabaka, Mb.,
Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia
Prof. Makame M. Mbarawa, Mb.,
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi
Prof. Anna K. Tibaijuka, Mb.,
Waziri wa Maji
Prof. Jumanne Maghembe, Mb.,
Waziri asiyekuwa na Wizara Maalum
Prof. Mark Mwandosya, Mb.,
Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika
Eng. Christopher Chiza, Mb.,
Waziri wa Uchukuzi
Dr. Harrison Mwakyembe, Mb.,
Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Dr. Fenella E. Mukangara, Mb.,
Waziri wa Maliasili na Utalii
Ndugu Khamis Kagasheki, Mb.,
Waziri wa Viwanda na Biashara
Dr. Abdallah O. Kigoda, Mb.,
Waziri wa Fedha
Dr. William Mgimwa, Mb.,
Waziri wa Nishati na Madini
Prof. Sospeter Muhongo, Mb.,
5. NAIBU MAWAZIRI
OFISI YA RAIS
HAKUNA NAIBU WAZIRI
6. OFISI YA MAKAMU WA RAIS
Naibu Waziri, Ofisi ya Makamu wa Rais
Ndugu Charles Kitwanga, Mb.,
7. OFISI YA WAZIRI MKUU
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Majaliwa K. Majaliwa, Mb.,
Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI)
Ndugu Aggrey Mwanry, Mb.,
8. WIZARA MBALIMBALI
Naibu Waziri wa Kazi na Ajira
Dr. Makongoro M. Mahanga, Mb.,
Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika
Ndugu Adam Malima, Mb.,
Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi
Ndugu Pereira A. Silima, Mb.,
Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara
Ndugu Gregory G. Teu, Mb.,
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Mifugo na Uvuvi
Ndugu Benedict N. Ole-Nangoro, Mb.,
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa
Ndugu Mahadhi J. Maalim, Mb.,
Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi,
Ndugu Goodluck J. Ole-Medeye, Mb.,
Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia na Watoto
Ndugu Ummy A. Mwalimu, Mb.,
Naibu Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi
Ndugu Philipo A. Mulugo, Mb.,
Naibu Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki
Dr. Abdulla Juma Abdulla, Mb.,
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii
Ndugu Lazaro Nyalandu, Mb.,
Naibu Waziri wa Ujenzi
Ndugu Gerson Lwenge, Mb.,
Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,
Dr. Seif Suleiman Rashid, Mb.,
Naibu Waziri wa Nishati na Madini
Ndugu George Simbachawene, Mb.,
Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia
Ndugu January Makamba, Mb.,
Naibu Waziri wa Uchukuzi
Dr. Charles J. Tizeba, Mb.,
Naibu Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni na Michezo
Ndugu Amos Makala, Mb.,
Naibu Waziri wa Maji
Eng. Dr. Binilith Mahenge, Mb.,
Naibu Waziri Nishati na Madini
Ndugu Stephen Maselle, Mb.,
Naibu Waziri wa Katiba na Sheria
Ndugu Angela Jasmine Kairuki, Mb.,
Naibu Waziri wa Fedha
Ndugu Janet Mbene, Mb.,
Naibu Waziri wa Fedha
Ndugu Saada Mkuya Salum, Mb.,
Imetolewa na:
Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu.
Dar es Salaam.
4 Mei, 2012
Tuesday, April 10, 2012
Wednesday, March 21, 2012
Maradhi ya Ajabu
MTOTO Honolata Juma Christian (8), (pichani) mkazi wa Mgeta wilayani Mvomero aliyetelekezwa na ndugu zake kutokana na maradhi ya ajabu yanayo msumbua, http://www.blogger.com/img/blank.gifanataabika katika hospitali ya rufaa mjini hapa akiomba msaada wa shilingi 1,000,000 ili akatibiwe.
Gharama hizo ni za tiba,usafiri na matumizi katika Hospitali ya KCMC ya mjini Moshi ambako ameshauriwa kwenda na madaktari wa hospitali ya Mkoa wa Morogoro alikolazwa.
Honolata ambaye tangu kuzaliwa kwake amekuwa akisumbuliwa na magonjwa likiwemo la kuota nywele mwili mzima, nundu mbili kichwani mithili ya pembe na matatizo ya macho.
Mtoto huyo analelewa na mama yake mzazi, Grace Francis (30) ambaye anadai ndugu zake wamemsusia na hawataki kumsaidia.
Monday, February 27, 2012
MAKAMU WA RAIS DKT BILAL AZINDUA JENGO LA WAKULIMA WA CHAI NA KITUO CHA MAFUNZO YA WAKULIMA WA CHAI RUNGWE MBEYA
Saturday, February 18, 2012
JK aongoza matembezi ya hisani kusaidia ujenzi wa hospitali ya kinamama ya CCBRT jijini Dar

Rais Kikwete akiongoza matembezi ya Hisani kuchangia ujenzi wa hospitali ya kinamama ya Baobab iliyo chini ya CCBRT jijini Dar es salaam. Katika picha kutoka kulia Meya wa Ilala Mh Jerry Silaa, Meya wa Kinondoni Mh Mwenda, Bw Erwin Telemans Mkurugenzi mtendaji wa CCBRT, Rene Meza Mkurugenzi Mtendaji wa Vodacom Tanzania, Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi ya CCBRT Bw. Wilbroad Slaa na kulia kwa Rais ni Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dr. Hadji Mponda na Mkurugenzi wa Vodafone Foundation Bw. Andrew Dunnet pamoja na Mwamvita Makamba wa Vodacom Tanzania katika matembezi hayo leo asubuhi.
JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA LAWAMANI KUHUSIKA NA KIFO CHA MWANACHUO ALIYE FARIKI SIKU YA WAPENDANAO YANI VALENTINE DAY
Marehemu Daniel Godluck Mwakyusa (31) ambaye ni mwanafunzi wa chuo cha TEKU aliyeuawa na Askari wa Jeshi la Polisi PC Maduhu tarehe 14/02/2012 katika sikukuu ya wapendanao {valentine day].
Habari na Ezekiel Kamanga, Mbeya.
Watu watatu wamefariki dunia mkoani MBEYA katika matukio matatu tofauti, likiwemo la tukio la Mwanafunzi wa chuo kikuu cha TEKU kilichopo jijini mbeya marehemu Daniel Godluck Mwakyusa (31) ambaye ni mwanafunzi wa chuo hicho aliuawa na Askari wa Jeshi la Polisi PC Maduhu tarehe 14/02/2012 katika sikukuu ya wapendanao {valentine day].
Marehemu akiwa na wenzake wanne walikuwa katika matembezi ambapo polisi walikuwa doria walikuta vijana hao wakipata vinywaji ndipo waliwatuhumu kuwa ni majambazi ambapo PC Maduhu alimpiga marehemu risasi mbili kwa kutumia bunduki aina ya [SMG].
Pia marehemu aliporwa shilingi laki tatu pamoja na simu ya mkononi .
Kwa mujibu wa baba mzazi wa marehemu huyo Bwana Pastory Mwakyusa amesema kuwa anasikitishwa sana na kitendo hicho kilichotokea kwani mwanawe hakuwa na tabia ya wizi au ujambazi hivyo ameliomba Jeshi la Polisi kueleza sababu ya kumuua mtoto wake.
Hata hivyo Jeshi la Polisi lilitoa usafiri wa gari lenye nambari za usajili T 138 AFK aina ya Coster kwa ajili ya kusafirisha Mwili wa marehemu kwenda katika wilaya ya Kyela kwa ajili ya mazishi baada ya uchunguzi wa daktari kuthibitisha kuwa marehemu ameuwawa kwa risasi.
Tukio la pili marehemu Zuberi Mwajeleba (21) mkazi wa kijiji cha Ibumba wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya ambaye alinyongwa kisha mwili wake kutupwa katika mto wa Kanyegele wilayani humo.
Kamanda wa polisi mkoani Mbeya Advocate Nyombi amesema chanzo cha tukio hilo bado hakijafahamika na Jeshi la Polisi linaendelea kufanya uchunguzi juu ya tukio hilo.
Katika tukio la tatu limetokea majira ya saa nane mchana katika eneo la Ilomba jijini Mbeya ambapo pikipiki yenye namba za usajili T 834 BOX aina ya Shinray ambayo dereva wake bado hajafahika alimgonga mtoto Mildred Immanuel (10) mkazi wa eneo hilo.
Hata hivyo dereva alitoroka na kuitelekeza pikipiki katika eneo la tukio na pikipiki hiyo imehifadhiwa katika Kituo cha kati cha Jeshi la Polisi, na mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa Jijini Mbeya na Polisi wanafanya juhudi za kumtafuta dereva huyo.
HABARI YA KUFUFUKA.
Wakati huo huo katika hali isiokuwa ya kawaida Roza Simbeye ambaye ni mama wa mtoto mmoja katika kitongoji cha Isandula, kijiji cha Vuwile, Kata ya Isandula, aliyefariki Februari 16 majira ya saa kumi na mbili za jioni amefufuka wakati taratibu zote za mazishi zipokamilika kama kuchimba kaburi na kuchonga jeneza na taratibu za ibada.
Na ilipofika majira ya saa 3:30 asubuhi ya Februari 17 baada ya kaburi kuchimbwa na jeneza kukamilika zilianza taratibu za kuchukua mwili wa marehemu Roza chumbani ndipo watu waliopewa jukumu la kumwosha walishangaa kumwona marehemu akiwa hai huku akiwa amtoa macho kama vile mtu ametoka usingizini ambapo mpaka sasa kaburi halijafukiwa wala jeneza halijatumiwa na kufanya wanakijiji kubaki na mshangao.
JESHI LA POLISI MKOANI MBEYA LAWAMANI KUHUSIKA NA KIFO CHA MWANACHUO ALIYE FARIKI SIKU YA WAPENDANAO YANI VALENTINE DAY
Happy Nenga ilivyotaka kutumaliza

Mungu ni mkubwa sana na bado anapenda niishi, hii ajali ckutegemea kama kuna mtu angepona, nilikuwa na kaka yangu tunatoka mbeya kuja dar siku hiyo... tumefika mitaa ya inyara (Tazama Pipeline) basi la ngangaline lilisimama njiani likipakia abiria na sisi tulikuwa kwenye mwendo wa kasi sana akashindwa kuova take ikabidi aliweke pembeni kwa kuseleleka na kukaa mkao huo..... but we are alive.
Monday, February 13, 2012
Saturday, February 4, 2012
We're better off than United, and Torres can prove it, says Villas-Boaz
Friday, January 27, 2012
BALAA! SERIKALI YASHUPAA MADAI YA MADAKTARI

Na. Aron Msigwa –MAELEZO
Serikali imewataka madaktari wote nchini walio kwenye mgomo kurejea katika vituo vyao vya kazi na kufanya kazi za utabibu ili kuokoa maisha ya wagonjwa.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es salaam waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dkt. Hadji Mponda amesema serikali inatambua mchango walio nao wataalam wa afya katika utoaji wa huduma za afya nchini na inaendelea kuboresha maslahi yao.
Amesema serikali kwa kutambua mchango huo imekuwa ikiboresha maslahi yao na kuongeza nafasi za ajira kila mwaka kwa wataalam wenye sifa kutoka nafasi 1,677 za mwaka 2005/2006 hadi kufikia 9,391 katika mwaka huu wa fedha 2011/2012.
“Serikali inatambua mchango wa watumishi wa kada za afya nchini na ndio maana nafasi za ajira zimekuwa zikiongezeka kila mwaka hasa katika mwaka huu wa fedha 2011/2012”
Amefafanu kuwa madaktari kupitia Chama chao (MAT) wamewasilisha madai mbalimbali serikalini yakiwemo nyongeza ya posho ya kuitwa kazini baada ya kazi na madaktari kupewa nyumba za kuishi karibu na hospitali amesema kuwa serikali imekuwa ikifanya jitihada za kuboresha maslahi hayo ili kuwawezesha wataalam hao kutekeleza majukumu yao ikiwemo ujenzi wa nyumba 8 za madaktari kwa wilaya 18 pamoja na kufanya maboresho ya posho.
“Serikali imepata fedha kutoka Mfuko wa Dunia(Global Fund) kwa ajili ya kujenga nyumba za madaktari na kwa kuanzia wilaya 18 zilizo pembezoni zimechaguliwa kujengewa nyumba 8 kila wilaya kama hatua ya kuboresha upatikanaji wa nyumba”
Kuhusu malipo ya udhamini kwa madaktari wanaochukua mafunzo ya uzamili,Kuhamisha madaktari bingwa wenye mikataba ya Ajira na Hospitali ya Taifa Muhimbili, Posho ya mazingira hatarishi na ajira za madaktari amesema kuwa baada ya serikali kupandisha hadhi ya hospitali za mikoa kuwa hospitali za Rufaa za mikoa kumekuwa na umuhimu wa madaktari hao kwenda kufanya kazi katika hospitali hizo na kuongeza kuwa idadi ya udhamini wa madaktari katika mafunzo ya uzamili imekuwa ikiongezeka mwaka hadi mwaka.
Aidha kuhusu madai ya kutaka nyongeza za mishahara ya shilingi milioni 3.5 kwa mwezi Dkt. Mponda ameeleza kuwa mishahara ya watumishi serikalini hufuata miundo ya utumishi (Scheme of Service)iliyopo huku akibainisha kuwa muundo wa malipo ya watumishi wa umma katika sekta ya afya umeboreshwa.
“Lazima tukubali kuwa baada ya kuboreshwa kwa miundo ya utumishi wa umma wafanyakazi wa sekta ya afya hivi sasa wanapata mishahara mikubwa kuliko watumishi wengine serikalini” amesisitiza.
MAKAMU WA RAIS DKT. BILAL ATEMBELEA MASHAMBA YA MPUNGA KOROGWE, AWEKA JIWE LA MSINGI JENGO LA UKUMBI NA OFISI YA HALMASHAURI YA KOROGWE

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka Jiwe la Msingi katika jengo jipya la Ukumbi na Ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Korogwe, wakati alipokuwa katika ziara yake ya kukagua miradi ya maendeleo ya Wilaya ya Korogwe mkoa wa Tanga jana Januari 26, 2012.
Majambazi yapanga mawe na kupora manyoni

Ndugu zangu,
Niliondoka Singida Mjini saa kumi na moja alfajiri kuelekea Dodoma. Kilomita 40 kutoka Manyoni nilikutana na hali hiyo pichani kunako saa kumi na mbili na nusu. Eneo la tukio niliwakuta askari watano wamevalia kiraia wakiwa na silaha za moto. Wameniambia tukio limetokea usiku wa kuamkia leo majira ya kuanzia saa sita usiku na linawahusisha maja majambazi wasiopungua wanane.
Kuna walioporwa fedha, simu na mali zao . Mahali hapa kuna pori kubwa upande wa kushoto. Inaaminika majambazi hayo yenye silaha yangali yamejiicha porini.
Hakuna aliyekamatwa. Nilishuhudia polisi hao wakifuatilia nyayo huku wakinionyesha mahali majambazi hayo yalilala chini kujificha wakisubiri giza na kuanza kupanga mawe yao. Kwa kusoma mazingira ya eneo kwangu mimi napata tafsiri kuwa majambazi hayo yalifanya maandzi ya mpango wao kwa siku kadhaa.
Maana, mawe hayo mazito yanaonekana kuwa yalikuwa yakisogezwa usiku karibu na tukio na kufikia idadi waliyohitaji. Intelijensia ya kipolisi ingefanya kazi yake sawa sawa na kwa kushirikiana na wenyeji ingewezeza kubaini mapema movement ya mawe yale. Na katika dunia ya sasa , mbwa wa polisi waliopewa mafunzo wangefanya kwa haraka na kwa ufanisi zoezi la kufuatilia majambazi porini badala ya polisi kufuatilia nyayo kwa macho
mtoto waua Mbeya
MWANAMKE ASHITAKIWA KWA KOSA LA KUSABABISHA KIFO CHA MWANAE
Habari na Mwandishi wetu
Neema Edson mwenye umri wa miaka 19 mkazi wa Namtanga Swaya jijini Mbeya amefikishwa katika mahakama ya mkoa kwa kosa la kumuua mtoto wake akiwa mchanga.
Akisoma shitaka hilo mbele ya hakimu mkazi mfawizi Monika Ndyekobola mwanasheria wa serikari Ema Msofe amesema mshtakiwa alitenda kosa hilo January 3 mwaka huu maeneo ya namtanga jijini hapa.
Amemtaja mtoto aliyeuawa kuwa Steven Chinga ambaye alikuwa na umri chini ya miezi kumi na miwili kinyume na kifungu cha sheria namba 199 sura ya 16 kama kilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.
Hata hivyo mshtakiwa hakutakiwa kujibu lolote kutokana na mahakama hiyo kutokuwa na dhamana ya kusikiliza kesi kama hizo na kesi hiyo itaanza kusomwa upya februari 6 mwaka huu katika mahakama kuu.
Neema Edson mwenye umri wa miaka 19 mkazi wa Namtanga Swaya jijini Mbeya amefikishwa katika mahakama ya mkoa kwa kosa la kumuua mtoto wake akiwa mchanga.
Akisoma shitaka hilo mbele ya hakimu mkazi mfawizi Monika Ndyekobola mwanasheria wa serikari Ema Msofe amesema mshtakiwa alitenda kosa hilo January 3 mwaka huu maeneo ya namtanga jijini hapa.
Amemtaja mtoto aliyeuawa kuwa Steven Chinga ambaye alikuwa na umri chini ya miezi kumi na miwili kinyume na kifungu cha sheria namba 199 sura ya 16 kama kilivyofanyiwa marekebisho mwaka 2002.
Hata hivyo mshtakiwa hakutakiwa kujibu lolote kutokana na mahakama hiyo kutokuwa na dhamana ya kusikiliza kesi kama hizo na kesi hiyo itaanza kusomwa upya februari 6 mwaka huu katika mahakama kuu.
Subscribe to:
Posts (Atom)